Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Lugola: Tutafika pahala, maiti zitachukuliwa hatua
Habari Mchanganyiko

Lugola: Tutafika pahala, maiti zitachukuliwa hatua

Kangi Lugola Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Spread the love

KANGI Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi amekemea uzembe wa baadhi ya askari polisi dhidi ya wahalifu wa ujambazi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Lugola ameeleza kuwa, uzembe huo ukikithiri itafikia pahala mamlaka husika zitaanza kuchukulia hatua maiti, za askari polisi atakaye zembea katika kupambana na wahalifu wa ujambazi.

“ Jambazi ambaye anakutana na Polisi kabla hajajiandaa kuwawahi Polisi, tayari awe amewahiwa zamani na kuangushwa chini. Na ninasema, Polisi ambaye atazembea zembea mpaka akawahiwa wakati na yeye ana mashine yake, tutafika pahala hata maiti sasa tuanze kuichukulia hatua,” amesema Lugola.

Lugola amesema kushughulika na majambazi sio sawa na kutongoza mwanamke, na kwamba lazima Polisi wawahi majambazi kabla hawajadhuru wananchi au wao wenyewe.

“Kushughulika na majambazi sio sawa na tunavyotongoza mwanamke. Unajua dada nakumaindi, unajua dada ulinipa namba ya bajaji. Hakuna, nimesema jambazi ambaye anakwenda kufanya ujambazi awahiwe kabla ya huyo jambazi hajamuwahi mwananchi,” amesema Lugola.

ReplyForward

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Songwe awafunda trafki kuzingatia uadilifu

Spread the loveASKARI wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Songwe wametakiwa kuendelea...

Habari Mchanganyiko

Mchimba madini jela maisha kwa kubaka, alihonga Sh 500

Spread the loveMahakama ya wilaya ya Songwe imemtia hatiani na kumhukumu kifungo...

Habari Mchanganyiko

Mlima wa Moto wazindua kongamano la SHILO kumuenzi Rwakatare

Spread the loveKANISA la Mlima wa Moto Mikocheni jijini Dar es Salaam,...

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

error: Content is protected !!