Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe apata ulinzi wa Polisi
Habari za Siasa

Mbowe apata ulinzi wa Polisi

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

JESHI la Polisi wilayani Hai mkoa wa Kilimanjaro, limevamia mkutano wa ndani wa Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni, kumlinda kiongozi huyo na wafuasi wake. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Tukio hilo limetokea leo tarehe 30 Septemba 2019 baada ya Lengai Ole Sabaya, Mkuu wa Wilaya ya Hai kuagiza polisi kufika katika mkutano huo, kwa ajili ya kufuatilia agenda zake.

Ole Sabaya ameeleza kuwa, amechukua hatua hiyo kwa ajili ya kumlinda Mbowe, viongozi na wafuasi wa Chadema waliohudhuria katika mkutano huo, uliofanyika katika ofisi za Chadema za Wilaya ya Hai.

Mkuu huyo wa wilaya amesema, wanaoshiriki katika mkutano huo, hawana sababu ya kutaharuki kama wamefanya mkutano huo kwa nia njema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!