FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Chadema Kanda ya Kaskazini kupitia ukurasa wake wa Twitter, Mbowe amekamatwa leo tarehe 28 Februari 2020, baada ya kumaliza kufanya mkutano wa hadhara jimboni kwake.
Taarifa ya kanda hiyo imedai kuwa, Polisi hawakueleza sababu za kumkamata Mbowe.
Mbowe alifanya mkutano wa hadhara katika viwanja vya Nkoromu kwenye Kata ya Masama, Wilayani Hai.
Leave a comment