Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mawasiliano ya barabara Dar mikoani yarejea
Habari Mchanganyiko

Mawasiliano ya barabara Dar mikoani yarejea

Spread the love

MAWASILIANO ya barabara kati ya jiji la Dar es Salaam na mikoani imerejea leo baada ya magari kuanza kupita katika daraja la Kiluvya ambalo jana lilikuwa limejaa maji na hivyo kufungwa kwa ajili ya usalama, anaandika Richard Makore.

Leo mtandao huu wa MwanaHALISI Online umeshuhudia mabasi yaendayo mikoani yakipita katika daraja hilo baada ya vyombo vya ulinzi na usalama kujiridhisha kwamba hakuna madhara yanayoweza kutokea hapo tena.

Jana vyombo hivyo viliyazuia magari yote kupita hapo na hivyo kuelekeza mabasi yaliyokuwa yakitokea mikoa mbalimbali ya bara kupita Bagamoyo ili kuingia jijini Dar es Salaam.

Mvua zilizonyesha juzi na jana mchana zilileta madhara baada ya daraja la Kiluvya linalounganisha mkoa wa Pwani na Dar es Salaam kuja maji na hivyo magari kushindwa kupita.

Kutokana na daraja hilo kujaa maji hudumza za usafiri wa magari ya abiria, mizigo na binafsi ulisitishwa na wananchi wakaombwa kutumia barabara ya Bagamoyo.

Daraja hilo ni kiungo muhimu kati ya jiji la Dar es Salaam pamoja na mikoa mbalimbali ya Kaskazini, Kati, Kanda ya Ziwa, Nyanda za juu Magharibu.

Aidha, mvua hizo zilisababisha maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam kujaa maji zikiwamo nyumba na kusababisha uharibifu wa mali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!