NCHI ya Burundi imekuwa ya kwanza kwa Afrika Mashariki kujiondoa uanachama katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Jinai (ICC).
Serikali ya taifa hilo la Afrika Mashariki ilitoa taarifa ya kusudio lao la kutaka kujindoa ICC kwa Umoja wa Mataifa (UN), kuhusu hatua hiyo mwaka mmmoja uliopita na leo inaweza kuruhusiwa rasmi kujiondoa.
Kulingana na mwandishi wa BBC, Anna Holligan kujiondoa kwa Burundi ni majuto makubwa.
Mahakama ya ICC imeanza kutathmini iwapo inaweza kuchunguza ghasia za kisiasa zilizoibuka baada ya rais Pierre Nkurunziza kuchukuwa madaraka kwa awamu ya tatu, licha ya kuwepo kwa kipindi cha mihula miwili katika katiba ya taifa hilo.
ICC bado ina uwezo wa kuchunguza uhalifu uliotekelezwa wakati Burundi ilipokuwa mwanachama wa mahakama hiyo.
Lakini haiwezi kuchunguza uhalifu wowote wa siku zijazo kwa kuwa haitakuwa tena mwanachama.
Hatua hiyo inaweza kuwa mfano na kuonyesha viongozi wengine kwamba kujiondoa katika mahakama hiyo ni njia mojawapo ya kuepuka jicho la kimataifa hadi pale jamii ya kimataifa itakapochukua hatua na taasisi kama vile Umoja wa
Afrika ama Baraza la Usalama la UN litakapowafuatilia washukiwa na kuyakumbusha mataifa kwamba kujiondoa katika ICC hakumaanishi moja kwa moja kwamba waathiriwa hawatopata haki.
Leave a comment