Sunday , 3 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Nkurunzinza aichomoa Burundi ICC
Kimataifa

Rais Nkurunzinza aichomoa Burundi ICC

Pierre Nkurunziza, Rais wa Burundi
Spread the love

NCHI ya Burundi imekuwa ya kwanza kwa Afrika Mashariki kujiondoa uanachama katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Jinai (ICC).

Serikali ya taifa hilo la Afrika Mashariki ilitoa taarifa ya kusudio lao la kutaka kujindoa ICC kwa Umoja wa Mataifa (UN), kuhusu hatua hiyo mwaka mmmoja uliopita na leo inaweza kuruhusiwa rasmi kujiondoa.

Kulingana na mwandishi wa BBC, Anna Holligan kujiondoa kwa Burundi ni majuto makubwa.

Mahakama ya ICC imeanza kutathmini iwapo inaweza kuchunguza ghasia za kisiasa zilizoibuka baada ya rais Pierre Nkurunziza kuchukuwa madaraka kwa awamu ya tatu, licha ya kuwepo kwa kipindi cha mihula miwili katika katiba ya taifa hilo.

ICC bado ina uwezo wa kuchunguza uhalifu uliotekelezwa wakati Burundi ilipokuwa mwanachama wa mahakama hiyo.

Lakini haiwezi kuchunguza uhalifu wowote wa siku zijazo kwa kuwa haitakuwa tena mwanachama.

Hatua hiyo inaweza kuwa mfano na kuonyesha viongozi wengine kwamba kujiondoa katika mahakama hiyo ni njia mojawapo ya kuepuka jicho la kimataifa hadi pale jamii ya kimataifa itakapochukua hatua na taasisi kama vile Umoja wa

Afrika ama Baraza la Usalama la UN litakapowafuatilia washukiwa na kuyakumbusha mataifa kwamba kujiondoa katika ICC hakumaanishi moja kwa moja kwamba waathiriwa hawatopata haki.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

error: Content is protected !!