Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Matokeo kidato cha sita haya hapa
ElimuTangulizi

Matokeo kidato cha sita haya hapa

Dk. Charles Msonde
Spread the love

BARAZA la Mitihani la Taifa (Necta) nchini Tanzania, limesema watahiniwa 82,440 sawa na asilimia 98.35 ya watahiniwa 84,212 waliofanya mtihani kidato cha sita Juni/Julai 2020 wamefaulu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea)

Akitangaza matokeo hayo visiwani Zanzibar leo Ijumaa tarehe 21 Agosti 2020, Katibu Mtendaji wa Necta, Dk. Charles Msonde amesema, watahiniwa 85,499 walisajiliwa kufanya mtihani huo.

Amesema, kati yao wasichana walikuwa 36,168 sawa na asilimia 42.30 na wavulana walikuwa 49,331 sawa na asilimia 57.70.

Dk. Msonde amesema, kati ya watahiniwa waliosajiliwa, watahiniwa wa shule walikuwa 74,753 na watahiniwa wa kujitegemea walikuwa 10,746.

Amesema, kati ya watahiniwa 85,499 waliosajiliwa kufanya mtihani huo, watahiniwa 84,212 sawa na asilimia 98.49 walifanya mtihani na 1,287 sawa na asilimia 1.51 hawakufanya mtihani huo kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo ugonjwa na utoro.

Katibu mtendaji huyo amesema, watahiniwa wa shule, kati ya 74,753 waliosajiliwa, watahiniwa 74,284 sawa na asilimia 99.37 walifanya mtihani ambapo wasichana walikuwa 32,403 sawa na asilimia 99.60 na wavulana 41,881 sawa na asilimia 99.19.

Amesema watahiniwa 469 sawa na asilimia hawakufanya mtihani.

 

Kuhusu watahiniwa wa kujitegemea, Dk. Msonde amesema, watahiniwa 10,746 walisajiliwa, watahiniwa 9,928 sawa na asilimia 92.39 walifanya mtihani na 818 sawa na asilimia 7.61 hawakufanya mtihani.

“Jumla ya watahiniwa 82,440 sawa na asilimia 98.35 ya watahiniwa waliofanya mtihani wa kidato cha sita wamefaulu.”

“Wasichana waliofaulu ni 35,486 sawa na asilimia 99.07 wakati wavulana waliofaulu ni 46,954 sawa na asilimia 97.81,” amesema Dk. Msonde.

Amesema, mwaka 2019, watahiniwa waliofaulu walikuwa 88,069 sawa na asilimia 98.32.

Kuhusu ubora wa ufaulu, Dk. Msonde amesema, madaraja waliyopata watahiniwa wa shule unaonyesha jumla ya watahiniwa 72,230 sawa na asilimia 97.74 wamefaulu kati ya darala la kwanza hadi la tatu wakiwemo wasichana 31,786 sawa na asilimia 98.24 na wavulana 40,444 sawa na asilimia 97.35.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!