Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Manara ang’aka Simba kupigwa sita Uturuki
Michezo

Manara ang’aka Simba kupigwa sita Uturuki

Spread the love

MSEMAJI wa Simba, Haji Manara amewashutumu vikali chombo cha Habari cha Clouds FM, kwa kutangaza taarifa za uongo kuhusu klabu ya Simba kucheza mchezo wa kirafiki na kufungwa mabao 6-0 nchini Uturuki ambayo timu hiyo imeweka kambi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Manara ameyasema hayo kupitia ukurasa wake kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram ambapo alikitaka chombo hicho cha habari kuthibitisha au kukanusha taarifa hiyo waliyoitoa yenye nia hovu ya kuidhalilisha klabu ya Simba.

Msemaji huyo wa Simba ameandika katika ukurasa wake maneno haya: “Ngugu zangu wa Clouds with do respect mnachotufanyia c haki na mnatokosea sana ten asana!! Leo mmetangaza kwenye radio yenu Simba imecheza mechi uturuki na kufungwa 6-0.. tunaomba mthibitishe au mkanushe … vinginevyo mtakuwa na nia ovu ya kutudhalilisha na kwa hili hatutawaelewa na hatutakubali!! Mm wajibu wangu pia ni kulinda image ya club yangu na sipo tayari kuona chombo chochote kikitangaza taarifa ya uzushi na uongo dhidi ya Simba kwa kisingizio chochote kile.. kwa hili nategemea mtachukua hatua stahiki haraka iwezekanavyo .. vinginevyo thibitisheni.”

Simba ambayo kwa sasa imeweka kambi nchini Uturuki kwa ajili ya kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara na Ligi ya Mabingwa Afrika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!