Friday , 26 April 2024
Habari za SiasaTangulizi

Makonda chali

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango (kulia), picha ndogo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alipokuwa anapokea makontena aliyoagiza
Spread the love

MPANGO wa Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuzuia kuuzwa makontena zaidi ya 20 yaliyoingizwa kwa jina lake kutoka nje, unaelekea kukwama. Anaripoti Regina Kelvin…(endelea).

Ni baada ya Dk. Phillip Mpango, Waziri wa Fedha na Mipango kusisitiza uuzwaji wa makontena hayo haraka.

Waziri Mpango ametoa agizo hilo leo tarehe 27 Agosti, 2018 alipofanya ziara ya kushtukiza katika bandari kavu iliyoko jijini Dar es Salaam.

Makonda amenukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini akilalamikia hatua ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuendesha mnada wa kuuza makontena hayo wiki iliyopita.

Akiwa bandarini hapo Waziri Mpango ameeleza kwa msisitizo kwamba, makontena hayo yanapaswa kupigwa bei haraka licha ya kuwepo kwa malalamiko ya mmiliki wake (Makonda).

Akisisitiza jambo hilo Waziri Mpango amesema kuwa, hatishwi na vitisho vya mwanasiasa huyo na ameapa kusimamia sheria na kanuni za kodi zilizoko hapa nchini.

Amesema lazima fedha za kodi kiasi cha Sh. 1.2 bilioni zinazodaiwa na TRA zinalipwa kwa mujibu wa sheria.

Makontena hayo yamebeba samani mbalimbali ikiwa ni mchango uliotolewa na Watanzania wanaoishi Marekani wanaojulikana kwa jina la Six Region Diaspora Council.

TRA ilipiga mnada makontena hayo ambapo mteja hakupatikana kutokana na kudaiwa kuuzwa kwa bei kubwa (milioni 60) wakati wateja walioendekeza mwisho iwe milioni 30.

Mnada huo unaendeshwa na Kampuni ya udalali ya Yono Action Mart. Hatua ya mnada inatokana na kushindwa kulipiwa kodi ya Sh. bilioni 1.2 zinazodaiwa na TRA baada ya kuwasili nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!