Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Majaliwa ahimiza viongozi wa dini kuhubiri amani
Habari Mchanganyiko

Majaliwa ahimiza viongozi wa dini kuhubiri amani

Spread the love

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewataka viongozi wa dini na Watanzania kwa ujumla watumie nyumba za ibada kuhubiri suala la amani na utulivu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Lindi…(endelea).

Taarifa iliyotumwa kwa umma na ofisi ya waziri mkuu imesema, Majaliwa ametoa wito huo leo Ijumaa tarehe 17 Julai 2020 wakati akizungumza na waumini wa dini ya Kiislamu alipohudhuria sala ya Ijumaa katika msikiti wa Buhari uliopo Ruangwa, mkoani Lindi.

Waziri mkuu amesema, ni muhimu Watanzania wakajenga tabia ya kuaminiana, kuvumiliana pamoja na kupendana kwani mambo haya yote huchangia uwepo wa amani na utulivu.

“Nchi hii imejizolea sifa kuwa ni nchi ya amani na utulivu kwa sababu jambo hili linahubiriwa na viongozi wa dini zote. Nchi hii sasa imekuwa ni kimbilio la nchi ambazo zimepoteza amani kwenye nchi zao, wanakuja hapa wanajifunza na wakirudi kwao wanaendelea kuwa salama,” amesema.

Majaliwa amesema, ni jukumu la kila Mtanzania kuzingatia mahubiri ya viongozi wa dini ili nchi iendelee kuwa na amani kwani kukiwa na amani na utulivu lazima maendeleo yataonekana.

“Nchi yetu imekuwa na kasi ya maendeleo katika maeneo mengi. Mimi naamini maendeleo haya yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na amani tuliyonayo na hii inatokana na mahubiri ya viongozi wetu wa dini. Dini ina mchango mkubwa sana katika uendeshaji wa Serikali,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!