Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Majaliwa ahimiza viongozi wa dini kuhubiri amani
Habari Mchanganyiko

Majaliwa ahimiza viongozi wa dini kuhubiri amani

Spread the love

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewataka viongozi wa dini na Watanzania kwa ujumla watumie nyumba za ibada kuhubiri suala la amani na utulivu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Lindi…(endelea).

Taarifa iliyotumwa kwa umma na ofisi ya waziri mkuu imesema, Majaliwa ametoa wito huo leo Ijumaa tarehe 17 Julai 2020 wakati akizungumza na waumini wa dini ya Kiislamu alipohudhuria sala ya Ijumaa katika msikiti wa Buhari uliopo Ruangwa, mkoani Lindi.

Waziri mkuu amesema, ni muhimu Watanzania wakajenga tabia ya kuaminiana, kuvumiliana pamoja na kupendana kwani mambo haya yote huchangia uwepo wa amani na utulivu.

“Nchi hii imejizolea sifa kuwa ni nchi ya amani na utulivu kwa sababu jambo hili linahubiriwa na viongozi wa dini zote. Nchi hii sasa imekuwa ni kimbilio la nchi ambazo zimepoteza amani kwenye nchi zao, wanakuja hapa wanajifunza na wakirudi kwao wanaendelea kuwa salama,” amesema.

Majaliwa amesema, ni jukumu la kila Mtanzania kuzingatia mahubiri ya viongozi wa dini ili nchi iendelee kuwa na amani kwani kukiwa na amani na utulivu lazima maendeleo yataonekana.

“Nchi yetu imekuwa na kasi ya maendeleo katika maeneo mengi. Mimi naamini maendeleo haya yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na amani tuliyonayo na hii inatokana na mahubiri ya viongozi wetu wa dini. Dini ina mchango mkubwa sana katika uendeshaji wa Serikali,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!