Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lugola achemka, JPM atumbua
Habari za SiasaTangulizi

Lugola achemka, JPM atumbua

Kangi Lugola, Waziri wa mambo ya Ndani. Picha ndogo wakati akiapishwa
Spread the love

LICHA ya maelezo na maelekezo ya mara kwa mara yanayotolewa na Kangi Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Jeshi la Polisi, polisi wake wameendelea kuogelea kwenye tuhuma nzito. Anaandika Mwandishi Wetu … (endelea).

Lugola amekua akitembelea maeneo mbalimbali nchini na kukutana na ‘vijana wake’ huku akitoa maelezo na kuonya watakaojihusisha na vitendo vya rushwa, unyanyasaji na ubambikiaji kesi lakini bado vitendo hivyo vinaendelea kumea kwenye jeshi hilo huku akishindwa kubaini.

Hatua hiyo imemsukuma Rais John Magufuli kuagiza kusimamishwa kazi Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Augustino Ollomi, Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Kyerwa, Justine Joseph.

Wengine wanaotakiwa kusimamishwa ni Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Kyerwa, Everist Kivuyo na Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Kyerwa, Robert Marwa kutokana na hujuma.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu usiku wa kuamkia leo imeeleza kuwa, viongozi hao wa Jeshi la Polisi katika wilaya hiyo wanatuhumiwa kuhusika katika magendo ya zao la kahawa.

“Rais amemwagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jeneral Jacob Kingu na Inspekta Generali wa Polisi, Simon Sirro kuhakikisha uchunguzi wa kina unafanyika na hatua stahiki zinachukuliwa endapo watabainika,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Tuhuma hizo zimebainika juzi wakati Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipokuwa ziarani wilayani humo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!