Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Lisu kupamba tamasha la injili
Habari MchanganyikoTangulizi

Lisu kupamba tamasha la injili

Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki
Spread the love

MWIMBAJI wa nyimbo za injili, John Lisu anatarajia kutikisa katika tamasha la uamsho lililoanza ambalo litashirikisha watui wote bila kujali itikadi za dini zao, anaandika Dany Tibason.

Katika mahojiano maalumu na gazeti hili Mchungaji kiongozi wa Kanisa la Tanzania Assemblies Of God (victory Christian center) DK. Huruma Nkone alisema wameandaa mkutano wa uamsho unaoshirikisha watu wote bila kujali utofauti wa madhehebu.

Akifafananua zaidi amesema mhubiri katika mkutano huo wa uamsho ni Askofu Yona Suleiman kutoka kiomboi mkoani Singida.

Tamasha hilo la uamsho litafanyika katika ukumbi wa Kanisa la Victory Christian Center na utafanyika jijini Dar es Salaam.

Amesema wakazi wa jiji la Dar es Salaam wanakabiribishwa ili kusikia neno la Mungu ambalo litatolewa na wahubiri mbalimbali.

“Ni kwa neema na waimbaji wengine watapamba mkutano huo wa uamsho ni Rivers of Joy International Kwaya ya Kanisa la KLPT Tageta na nyingine nyingi”alieleza Dk.Nkone.

DK Nkone ametoa wito kwa wakazi wa jiji la Dar kujitokeza kwa wingi kwani huduma ya maombi na maombezi itatolewa bure.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!