Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu: Rais Magufuli amebakiza siku 14 Ikulu
Habari za SiasaTangulizi

Lissu: Rais Magufuli amebakiza siku 14 Ikulu

Spread the love

MGOMBEA Urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amesema, Rais John Pombe Magufuli amebakisha siku 14 kubaki Ikulu, kwa kuwa hatoshinda katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Lissu ametoa kauli hiyo leo Jumatano tarehe 14 Oktoba 2020 wakati anazungumza na wananchi wa Kisiwa cha Ukerewe mkoani Mwanza, kuhusu changamoto wanazopitia kwenye sekta ya uvuvi katika mkutano wake wa kampeni.

Rais Magufuli anatetea kiti chake cha Urais kwa mara ya pili kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambapo aliingia madarakani tarehe 5 Novemba 2015 baada ya kushinda Uchaguzi Mkuu.

“Magufuli amebakisha wiki mbili Ikulu, tarehe 28 Oktoba 2020 tunawashinda, uchaguzi ukiisha hana kazi,” amesema Lissu.

Akizungumzia ahadi zake, Lissu amesema akichaguliwa kuwa Rais wa Tanzania, manyanyaso dhidi ya wananchi hasa wavuvi yatakuwa mwisho.

Amesema, ataunda tume itakayohusisha majaji wa mahakama za juu kuchunguza matukio ya unyanyasaji dhidi ya wavuvi.

“Jambo la kwanza kabisa kuhusiana na hili, kama rais wenu nitaunda tume ya majaji wa mahakama za juu kuchunguza matukio yote ya kuumiza watu, ya kutia watu umasikini ambayo yamefanyika katika mwambao wa Ziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa. Sababu kote nilipopita wavuvi ni kilio kikubwa,”amesema Lissu.

Lissu amesema, lengo la uundwaji wa tume hiyo ni kufahamu watu waliohusika na matukio ya unyanyasaji wa wavuvi, kwa ajili ya kuwachukulia hatua waliohusikanayo.

Pia, Lissu ameahidi kuziboresha sheria za uvuvi, kupanua bandari ya Nansio Ukerewe pamoja na kujenga daraja litakalounganisha kisiwa cha Kisorya mkoani Mara na Ukerewe mkoani Mwanza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!