Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lipumba, Maalim Seif siku zinahesabika
Habari za SiasaTangulizi

Lipumba, Maalim Seif siku zinahesabika

Spread the love

KESI ya Madai Na. 21 ya mwaka 2017 iliyopangwa kusikilizwa leo katika Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam, mbele ya Jaji Wilfred Dyansobera kuhusu wizi wa Sh. 369 milioni, fedha za ruzuku za Chama cha Wananchi – CUF imeahirishwa mpaka tarehe 10, Julai 2017, anaandika Hamisi Mguta.

Kesi hiyo ilifunguliwa na Bodi ya wadhamini wa CUF, ambapo  watuhumiwa ni pamoja na Jaji Francis Mutungi, Msajili wa Vyama vya Siasa, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa chama hicho anayetambulika na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa huku akiwa amefukuzwa uanachama na CUF.

Katika kesi hiyo jopo la mawakili wa upande wa mashtaka linaongozwa na Juma Nassoro, Daim Halfan na Hashimu Mzirai, upande wa utetezi unawakilishwa na mawakili ni Gabriel Malata ambaye ni Wakili wa Serikali Mkuu na Makubi Kunju, wakili wa upande wa Lipumba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!