Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lema kupishana na Mbowe jela?
Habari za Siasa

Lema kupishana na Mbowe jela?

Spread the love

GODBLESS Lema, Mbunge wa Iringa Mjini anaweza kupishana na mwenyekiti wake (Chadema) Freeman Mbowe, iwapo Biswalo Mganga, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) ‘atamkomalia.’ Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Mbowe yupo katika gereza la Segerea baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kumuhukumu kulipa faini au kutumikia kifungo cha miezi mitano jela kutokana na kesi yake ya uchochezi pamoja na viongozi wenzake wa Chadema.

Biswalo amesema, Lema aliudanganya umma kutokana na kusambaza taarifa za uongo kuhusu mauaji ya watu 14 wilayani Manyoni, Singida.

“Kwa hili lazima nitachukua hatua, hatuwezi kuendelea na upotoshaji na uvunjifu wa namna hii,” amesema Biswalo na kuongeza “halafu watu wanatoka na kusema, wanasiasa wa upinzani wanaonewa wakati wanafanya upuuzi wa namna hii.”

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 12 Machi 2020, jijini Dar es Salaam Biswalo amesema, Lema alitoa taarifa za uongo wakati alipohudhuria kwenye mazishi ya Alex Joas, katibu wa chama hicho Jimbo la Singida Mashariki.

Mwili wa Joas ulikutwa umetelekezwa kando ya barabara huku ukiwa na majeraha sehemu za kichwa.

“Mtaziona hatua nitazochukua. Nazifahamu mimi na ofisi yangu, hazitafanyika kwa kificho,” amesema Biswalo na kuongeza nimepitia jalada moja baada ya jingine, nimebaini polisi wamezifanyia kazi taarifa hizo tofauti na maelezo ya Lema.”

Amesema, pamoja na wanasiasa kukata kutumia matukio kisiasa, ni bora kukawa na mipaka akifafanua kwamba wengine vifo vyao vinasababishwa na ajali.

“…kuna marehemu mwingine vifo chao vimesababishwa na ajali ya pikipiki, lakini mheshimiwa Lema katika taarifa yake amesema amechinjwa. Mwingine alishambuliwa na fimbo, mateke na ngumi lakini anataja wamechinjwa, huu ni uongo,” amesema Mganga.

Amesema, serikali inapochukua hatua, ni vema wananchi wakatuelewa na kwamba, taifa hili haliwezi kuendelea kuwa la watu wazushi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!