SAED Kubenea, Mbunge wa Ubungo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) amesema kuwa, hakuna wa kumng’oa ndani ya chama hicho. Anaandika Faki Sosi…(endelea).
Kubenea ametoa kauli hiyo baada ya kuulizwa na waandishi wa habari kuhusu taarifa za kutajwa kutaka kuondoka kwenye chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“Hizi taarifa zimeenezwa na baadhi ya watu wakiwemo ndani ya Chadema kwa maslahi wanayoyajua wao na watu hao wanajulikana.
“Mimi niende CCM kwa lipi” amehoji na kuongeza; “mimi bana sitoki Chadema na hakuna wa kunitoa Chadema, nitabaki humo huko,” ameseam Kubenea.
Amesema kuwa, kuhusishwa kwake na kuhama kwa Mwita Waitara aliyekuwa Mbunge wa Ukonga aliyejiunga na CCM wiki iliyopita sio sahihi.
Ameeleza kuwa, hatua ya Mwita kuhamia CCM sio sahihi kwa kuwa wananchi wa Ukonga walimwamini na kumchagua kwa kura nyingi “hivyo alipaswa kupambana akiwa ndani ya Chadema.”
Kubenea amesema kuwa, atapambana ndani ya Chadema na akishindwa ataendelea na kazi yake ya uandishi.
Leave a comment