Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea: Hakuna wa kuning’oa Chadema
Habari za Siasa

Kubenea: Hakuna wa kuning’oa Chadema

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo
Spread the love

SAED Kubenea, Mbunge wa Ubungo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) amesema kuwa, hakuna wa kumng’oa ndani ya chama hicho. Anaandika Faki Sosi…(endelea).

Kubenea ametoa kauli hiyo baada ya kuulizwa na waandishi wa habari kuhusu taarifa za kutajwa kutaka kuondoka kwenye chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Hizi taarifa zimeenezwa na baadhi ya watu wakiwemo ndani ya Chadema kwa maslahi wanayoyajua wao na watu hao wanajulikana.

“Mimi niende CCM kwa lipi” amehoji na kuongeza; “mimi bana sitoki Chadema na hakuna wa kunitoa Chadema, nitabaki humo huko,” ameseam Kubenea.

Amesema kuwa, kuhusishwa kwake na kuhama kwa Mwita Waitara aliyekuwa Mbunge wa Ukonga aliyejiunga na CCM wiki iliyopita sio sahihi.

Ameeleza kuwa, hatua ya Mwita kuhamia CCM sio sahihi kwa kuwa wananchi wa Ukonga walimwamini na kumchagua kwa kura nyingi “hivyo alipaswa kupambana akiwa ndani ya Chadema.”

Kubenea amesema kuwa, atapambana ndani ya Chadema na akishindwa ataendelea na kazi yake ya uandishi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!