Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Kocha Mkuu Simba: Kundi letu lipo wazi
Michezo

Kocha Mkuu Simba: Kundi letu lipo wazi

Patrick Aussems, Kocha Mkuu wa Simba
Spread the love

KOCHA Mkuu wa Simba, Patrick Aussems amsema kuwa bado timu yake inanafasi ya kusonga mbele kwenye hatua ya robo fainali ya michuano ya Klabu Bingwa barani Afrika kutokana na kundi hilo kuonekana lipo wazi kwa timu yoyote kuweza kusonga mbele. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Kocha huyo amesema hayo kupitia kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter mara baada tu Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika CAF kupanga makundi hayo ya ligi ya mabingwa na Simba kuangukia kwenye kundi D, sambamba na klabu za Al Ahaly (Misri), As Vital (Congo DRC) na JS Saoura (Algeria).

“Kundi hili lipo wazi :Michezo ya kusisimua!! … Na kiukweli tunanafasi nzuri ya kufika robo fainali, kwa hiyo tunahitaji kuwa pamoja.”

Makundi hayo yalipangwa jana kwenye mji wa Cairo, Misri yalipo makao makuu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) ambapo Simba iliwakilishwa na mjumbe wa Bodi ya wakurugenzi wa klabu hiyo, Salim Abdallah ambapo mchezo wao wa awali wataanzia nyumbani Dhidi ya JS Saoura ya nchini Algeria.

Simba imefuzu kwenye hatua hii mara baada ya kuwatoa klabu ya Nkana FC kutoka nchini Zambia kwa jumla ya mabao 4-3 katika michezo yote miwili waliocheza nyumbani na ugenini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!