Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kituo cha kuzalisha umeme Mlandizi chateketea
Habari Mchanganyiko

Kituo cha kuzalisha umeme Mlandizi chateketea

Spread the love

KITUO cha kuzalisha na kusambaza umeme cha Mlandizi mkoani Pwani, kimteketea kwa moto leo tarehe 30 Machi 2019. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Akizungumza na MwanaHALISI ONLINE kuhusu tukio hilo, Wankyo Nyigesa, Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani amesema, moto huo ulizuka majira ya saa 2.15 asubuhi. 

Kamanda Wankyo amesema, hadi sasa chanzo cha moto huo hakijajulikana na kwamba, moto huo umeteketeza transform moja yenye megawati 24 ambayo ilikuwa ikizalisha na kusambaza umeme katika maeneo ya Bagamoyo, Kibaha na Mloganzila.

“Nikikuwepo eneo la tukio, hakuna madhara yoyote kwa binadamu isipokuwa jenereta limeteketea.  Hadi sasa chanzo cha ajali hiyo hakijajulikana, tunasubiri matokeo ya uchunguzi wa watalaamu,” amesema Kamanda Wankyo.


                                    

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!