Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kimenuka Waislamu na serikali
Habari za Siasa

Kimenuka Waislamu na serikali

Spread the love

MGOGORO mkubwa unafukuta kati ya serikali na viongozi wakuu wa madhehebu ya kiislamu mkoani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu.

Mgogoro unatokana na hatua ya mkuu wa mkoa wa Rukwa, Joachim Wangabo, kuzuia ujenzi wa msikiti wa kisasa mkoani humo.

Wakizungumza baada ya kumalizika swala ya Ijumaa mwishoni mwa wiki, mmoja wa viongozi wa kiislamu mkoani Rukwa amesema, “serikali inawabagua waislamu na hivyo hawana imani nayo.”

“Tunabaguliwa na serikali. Hivyo basi, hatuna imani nayo. Tunanyanyaswa kwenye nchi yetu. Hatuko tayari kushirikiana na serikali inayotubagua,” ameeleza sheikh huyo kwa sauti ya hasira.

Ameongeza, “hata leo sikwenda kwenye kikao cha RCC (kamati ya ushauri ya mkoa). Siwezi kwenda kwa kuwa mkuu wa mkoa ambaye ndiye mwenyekiti wa kikao hicho, amewadhalilisha viongozi wangu wa kiislamu.”

Anasema, hawezi kwenda kwenye mkutano huo kwa kuwa mkuu wa mkoa amesheheni kiburi; ametaka waislamu wote kutohudhuria vikao vya kamati za kata na wilaya.

Kufuatia hatua hiyo, taarifa zinamnukuu kiongozi huyo wa kidini akiagiza waislamu wote kujiweka tayari, ili kutekeleza alichoita, “maelekezo” yatakayotolewa na viongozi wao wa misikiti.

“Kwa sasa, tulieni kidogo. Subiri mpaka Jumatano ijayo. Baada ya hapo, maimamu wenu watatoa kauli. Naomba ikitolewa hiyo kauli, mutekeleze mtakachoambiwa,” ameeleza.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, hatua ya mkuu wa mkoa huo kuzuia ujenzi wa msikiti na kutaka kubomolewa inafuatia madai kuwa umejengwa mjini na hivyo unaleta kelele kwa watu ambao siyo waislamu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!