Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kaya 80 Dodoma zapokea msaada wa Mil 21
Habari Mchanganyiko

Kaya 80 Dodoma zapokea msaada wa Mil 21

Spread the love

JUMLA ya kaya 80 za wakazi wa Kata ya Chamwino Jijini Dodoma wamenufaika na msaada wa chakula na mahitaji mbalimbali kutoka, taasisi ya Dar-Ul-Muslimeen kwa kushirikiana na W.I.P.A.H.S. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Msaada huo wa chakula na mahitaji mbalimbali wenye thamani ya sh. 21 milioni utawalenga waumini wa dini ya Kiislam ambao wanatoka kaya zenye mahitaji maalumu ili ziweze kujikimu wakati wa kipindi cha Mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Ajira na Vijana na Watu wenye Ulemavu, Athony Mavunde, akipokea msaada huo  ameziomba taasisi za dini, mashirika ya umma na watu binafsi kusaidia watu wenye mahitaji maalumu hususani katika kipindi ambacho kuna janga la virusi vya ugonjwa wa corona.

Aidha kutokana na mlipuko wa virusi vya coron nchini, amewaomba wadau mbalimbali kuwasaidia waumini wasiojiweza wa dini ya kiislamu misaada ya vyakula vitakavyo wawezesha kutimiza moja ya nguzo ya dini hiyo.

Ushauri huo ametoa baada ya kupokea misaada ya chakula wenye thamani ya million 21 uliotolewa na taasisi hizo kwa waumini wa msikiti wa Hudda Chamwino jijini Dodoma.

Mavunde alisema kuwa katika kipindi hiki cha janga la ugonjwa wa corona kuna makundi mengi yanahitaji kusaidiwa mahitaji maalumu ikiwemo vifaa vya kujikinga na gonjwa hili.

Naibu Waziri huyo alisema kuwa ni wakati wa kutoa misaada ya vyakula kwa waumini wa dini ya kiislamu wanapoendea mwezi mtukufu ramadhani,ili waweze kujimudu kwa mguzo muhimu ya Uislamu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Dar-Ul-Muslimeen, Shekhe Muslim Bhanji, alisema kuwa jumla ya mifuko 300 ikiwemo mchele, maharange, sukari imetolewa kwa ajili ya kuwasaidia waumini wenye mahitaji maalumu wa msikiti wa Hudda wa Chamwino.

Pamoja na kusaidia kujikimu kwa Mwezi Mtukufu waumini waliopata msaada huo hawataweza kutembea  kutafuta mahitaji ikiwa ni pamojana kujikinga na maambukizi ya coroma.

Naye kwa upande wake Diwani wa kata hiyo ya Chamwino, Jumanne Gende (CCM) aliwataka waumini waliokabidhiwa misaada hiyo kuitumia kwa malengo yaliyokusudiwa  kutoka kwa wahisani hao.

Juma Kemo, Shekhe wa msikiti huo wa Hudda Chamwino akishukuru kwa kupatiwa msaada huo kwa niaba ya walengwa aliwataka kuuthamini huku pia wakijilinda na janga la maambukizi ya ugonjwa wa corona kwa kufuata maelekezo ya waatalamu wa afya na viongozi wa serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!