Sunday , 3 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Wanywaji pombe za kienyeji waonywa
Habari Mchanganyiko

Wanywaji pombe za kienyeji waonywa

Spread the love

DIWANI wa kata ya Ipagala jijini Dodoma, Doto Gombo, amewaonya wanywaji wa pombe za kienyeji kuacha tabia ya kuchangia chombo kimoja maarufu kwa jina la Chitochi. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Diwani huyo alisema kuwa wanywaji wengi wa pombe za kienyeji wanatabia ya kuchangia chombo kimoja zaidi ya watanohadi kumi jambo ambalo ni hatarikwa afya zao.

“Nipende kusema kuwa marufuku hiyo si kwa wanywaji wa pombe ya kienyeji tu hata wavuta sigara wanatabia ya kugongeana jambo ambalo kimsingi ni baya na linaweza kuchangia maambukizi ya Virusi vya Corona,” alisema Gombo.

Kuhusu wauzaji wa pombe majumbani alisema kuwa wanatakiwa kuzingatia usafi na taratibu zinazotakiwa ikiwa ni pamoja na kuvaa barakoa, maji tililika na sabuni pamoja na vitakasa mikono.

Katika hatua nyingine alisema wanywaji wa pombe hizo wanatakiwa kujiepusha na msongamano usiokuwa wa lazima.

“Kutokana na hali ilivyo kwa sasa mtumiaji wa pombe za kienyeji anatakiwa kutumia chombo chake na siyo kuchangiana,” alisema Diwani.

Gombo ametoa tahadhali hiyo alipokuwa akitoa maelekezo kwa watendaji, wenyeviti na mabalozi wa mitaa kuhakikisha vilabu vya pombe za kienyeji na wanaouzia majumbani wanachukua tahadhali kuepukana na maambukizi ya ugonjwa huo ikiwemo na wao wenyewe.

Alisema katika kipindi hiki cha ugonjwa kila maeneo yanatakiwa kuchukuliwa tahadhali kubwa ya kujilinda na hakuna sababu ya kubembelezana ikiwemo huko kwenye vilabu vya pombe za kienyeji.

Alisema wenye vilabu hivyo wanatakiwa kuhakikisha wanakuwa na vyombo safi vinavyotumika kunywea na vinakuwa vingi na siyo vya kupokezana kwa kila mnywaji na wakifanya hivyo wanaweza kuwa chanzo kuenea kwa gonjwa hilo hatari.

“Niwatake sasa hao wenye vilabu vya pombe na wale wanaouzia majumbani,wahakikishe wanakuwa na vyombo vya kutosha, na maeneo yao kuna vifaa vya kujilinda kama vile barakoa,maji na sabauni na vitakasa mikono,” alisema.

Diwani huyo hata hivyo amewataka wakazi wa kata hiyo kila kaya kunakuwa na vifaa vya kujilinda wao wenyewe ikiwemo madumu ya maji na sabani, vitakasa mikono na barakoa.

Alisema kutokana na kuwepokwaugonjwa wa Corona hakuna sababu ya kuoneana aibu bali kila kaya inatakiwa kutekeleza maagizo yanayotolewa na wataalamu wa Afya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

ElimuHabari Mchanganyiko

CEO NMB awataka vijana kunoa ujuzi wao

Spread the loveAfisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, amewashauri...

Habari Mchanganyiko

TARURA kujenga madaraja 189 kwa teknolojia ya mawe

Spread the loveWakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imejipanga kujenga...

AfyaHabari Mchanganyiko

Majaliwa aipongeza GGML mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveWaziri Mkuu Kassim Majaliwa ameipongeza Kampuni ya Geita Gold Mining...

error: Content is protected !!