Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM apiga kijembe Chadema
Habari za Siasa

JPM apiga kijembe Chadema

Safu mpya ya Uongozi wa Chadema
Spread the love
RAIS John Magufuli na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), ‘amerusha dongo’ kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) akisema, ‘kukimbia changamoto ni uoga.’ Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Tarehe 1 Mei 2020, Chadema kiliagiza wabunge wake kujiweka karantini kwa muda wa siku 14, ili kujichunguza kama wameambukizwa virusi vya Ugonjwa wa Homa Kali ya Mapafu vya Corona (Covid-19). Wabunge hao walirejea bungeni tarehe 15 Mei 2020.

Bila kutaja jina la chama hicho, Rais Magufuli katika hotuba yake ya kulifunga Bunge la 11 leo tarehe 16 Juni 2020, jijini Dodoma amesema, ‘kukimbia’ Bunge haikuwa ishara njema.

“Nafahamu wako wachache walikimbia, na sijui kama wamesharejea lakini niseme tu kwamba kukimbia halikuwa jambo sahihi, sababu matatizo au changamoto hazikimbiwi, kukimbia changamoto ni ishara ya udhaifu, lakini pia ni ishara ya woga, lakini pia ni ishara ya kutojiamini.

“Siku zote, njia sahihi ya kukabiliana na matatizo ni kuyakabili, na hii ndio sababu sisi tuliamua kakabiliana na corona huku tukimtanguliza Mungu. Kwa kufanya hivyo, tumeweza mpaka sasa hivi kutatua kwa kiasi kikubwa,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!