Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko JP DECAUX, Polisi waandaa tamasha la bodaboda 
Habari Mchanganyiko

JP DECAUX, Polisi waandaa tamasha la bodaboda 

Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Mwanza kwa kushirikiana na Kampuni ya JP DECAUX imeandaa tamasha la UNITY FESTIVAL kati ya bodaboda na askari Polisi  wa usalama barabarani litakalokuwa linatoa elimu na kuhamasisha kuzingatia sheria na usalama wa barabara. Anaripoti Moses Mseti, Mwanza … (endelea).

Hatua hiyo inakuja baada ya kuwepo kwa ajali za barabarani zisizokuwa za lazima zinazosababishwa na madereva wa pikipiki maarufu kama bodaboda.

Mratibu wa tamasha hilo kutoka kampuni ya JP DECAUX, (jp dikox), Anna Lukolongo alisema lengo la shindano hilo ni kutoa elimu kwa bodaboda hao pamoja na kuimalisha umoja kati yao na askari Polisi jijini hapa.

Lukolongo alisema katika tamasha hilo, michezo itakayofanyika siku hiyo (Julai 20, 2019) ni pamoja na mwendashaji mwenye stamina, anayeweza kupita kwenye vikwazo mbalimbali.

Alisema mshindi katika shindano hilo, atapata zawadi ya pikipiki mpya huku washiriki wote wakipatiwa elimu ya usalama barabarani ili kupunguza ajali zilizokuwa za lazima.

Aidha Lukolongo amesema bonanza hilo litanguliwa na michezo mbalimbali,ikifuatiwa na shindano la kumpata mwendashaji bora wa bodaboda itakayosimamiwa na askari wa usalama barabarani.

Tamasha hilo limebebwa na kauli mbiu isemayo ‘SOTE NI NDUGU,’ ambapo tayari limefanyika katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha na Morogoro ikiwa ni mwendelezo wa matamasha yaliyofanyika ya kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na China.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!