Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Isaya Mwita: Aliyeng’olewa Umeya wa Jiji, ageukia urais
Habari za Siasa

Isaya Mwita: Aliyeng’olewa Umeya wa Jiji, ageukia urais

Mwita Isaya, aliyekuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam akikabidhiwa fomu ya kugombea Urais katika Uchaguzi Mkuu 2020 kwa tiketi ya Chadema
Spread the love

MIEZI sita baada ya kung’olewa Umeya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).

Isaya amejitokeza leo kwenye ofisi za chama hicho zilizopo Mtaa wa Ufipa, Kinondoni jijini Dar es Salaam, na kukabidhiwa fomu hiyo na Reginald Munisi, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa chama hicho.

Isaya alitangazwa kuvuliwa umeya tarehe 9 Januari 2020, kwa madai mbalimbali.

Miongoni mwa tuhuma zake ni pamoja na kushindwa kuongoza kikao cha baraza la madiwani na kupendelea baadhi ya mameya kuingia katika kamati za fedha.

Alituhumiwa kuwa na matumizi mabaya ya gari umma kwa kulisababishia kupata ajali, jambo ambalo meya amekuwa akijibu kwamba yeye siyo dereva wa gari hilo.

Lakini pia kutotumia kiasi cha Sh. 5.8 bilioni, zilizotokana na mauzo ya hisa za Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), ambalo lilikuwa mali ya jiji.

Mwita Isaya, aliyekuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam akionyesha fomu ya kugombea Urais katika Uchaguzi Mkuu 2020 kwa tiketi ya Chadema

Isaya amechukua fomu leo tarehe 9 Julai 2020, Makao Makuu ya Chadema, Mtaa wa Ufipa jijini Dar es Salaam.

Mara baada ya kuchukua fomu hiyo, Isaya amesema kitu cha kwanza kwenye utawala wake ni Katiba Mpya kwa manufaa ya Watanzania wote.

“Katiba Mpya ndio jambo la kwanza nitakaloanza nalo endapo chama changu kitaniamini na kunipitisha na hatimaye kuwa Rais wa Tanzania, Katiba itaheshimiwa na kila mtu” amesema Isaya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!