Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Idadi ya wagonjwa wa corona yapaa
AfyaHabari MchanganyikoTangulizi

Idadi ya wagonjwa wa corona yapaa

Spread the love

WAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu ametangaza ongezeko la wagonjwa wa homa ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona nchini kutoka 53 hadi 88 baada ya wagonjwa wapya 29. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Ummy leo Jumatano Aprili 15, 2020, inaeleza wagonjwa hao wamebainika baada ya kutoka majibu ya sampuli zilizopimwa maabara Aprili 14 na 15, 2020.

Inaeleza kuwa wagonjwa wote ni Watanzania, kati yao 26 wapo Dar es Salaam, wawili Mwanza na mmoja mkoani Kilimanjaro.

“Wote wanaendelea na matibabu chini ya uangalizi wa wataalam wa afya. Ufuatiliaji wa watu waliokuwa karibu na wagonjwa hawa unaendelea,” amesema Ummy.

Inaeleza hadi leo watu 88 wamepata maambukizi kutoka watu 53 waliotolewa taarifa awali.

“Ongezeko hili la wagonjwa linajumuisha wagonjwa wapya sita waliotolewa taarifa mapema leo na Waziri wa Afya Zanzibar (Hamad Rashid). Aidha wagonjwa waliopona hadi leo ni 11 na vifo ni vinne,” anaeleza Ummy.

Ummy amesema Serikali inaendelea kuwataka wananchi kuchukua tahadhari ya kujikinga na ugonjwa huo kama wanavyopatiwa elimu mara kwa mara kupitia njia mbalimbali.

“Katika kipindi hiki ni muhimu kwa wananchi kuepuka misongamano na mikusanyiko isiyokuwa ya lazima. Ninawasihi wananchi kuacha kutoa taarifa za upotoshaji juu ya ugonjwa huu kwa kuwa zinaweza kuzua taharuki katika jamii,” amesema Ummy.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!