Thursday , 7 December 2023
Home Kitengo Maisha Afya Idadi ya wagonjwa wa corona yapaa
AfyaHabari MchanganyikoTangulizi

Idadi ya wagonjwa wa corona yapaa

Spread the love

WAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu ametangaza ongezeko la wagonjwa wa homa ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona nchini kutoka 53 hadi 88 baada ya wagonjwa wapya 29. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Ummy leo Jumatano Aprili 15, 2020, inaeleza wagonjwa hao wamebainika baada ya kutoka majibu ya sampuli zilizopimwa maabara Aprili 14 na 15, 2020.

Inaeleza kuwa wagonjwa wote ni Watanzania, kati yao 26 wapo Dar es Salaam, wawili Mwanza na mmoja mkoani Kilimanjaro.

“Wote wanaendelea na matibabu chini ya uangalizi wa wataalam wa afya. Ufuatiliaji wa watu waliokuwa karibu na wagonjwa hawa unaendelea,” amesema Ummy.

Inaeleza hadi leo watu 88 wamepata maambukizi kutoka watu 53 waliotolewa taarifa awali.

“Ongezeko hili la wagonjwa linajumuisha wagonjwa wapya sita waliotolewa taarifa mapema leo na Waziri wa Afya Zanzibar (Hamad Rashid). Aidha wagonjwa waliopona hadi leo ni 11 na vifo ni vinne,” anaeleza Ummy.

Ummy amesema Serikali inaendelea kuwataka wananchi kuchukua tahadhari ya kujikinga na ugonjwa huo kama wanavyopatiwa elimu mara kwa mara kupitia njia mbalimbali.

“Katika kipindi hiki ni muhimu kwa wananchi kuepuka misongamano na mikusanyiko isiyokuwa ya lazima. Ninawasihi wananchi kuacha kutoa taarifa za upotoshaji juu ya ugonjwa huu kwa kuwa zinaweza kuzua taharuki katika jamii,” amesema Ummy.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

RAS Songwe: Tumepigwa… mkurugenzi nakupa siku 21

Spread the loveKATIBU tawala mkoani Songwe, Happines Seneda ametoa siku 21 kwa...

Habari Mchanganyiko

Shura ya Maimamu kukata rufaa kupinga Sheikh kufungwa miaka 7

Spread the loveSHURA ya Maimamu Tanzania, inakusudia kukata rufaa dhidi ya hukumu...

BiasharaTangulizi

Bei ya Dizeli, Petroli yashuka

Spread the loveBEI ya mafuta kwa mwezi Disemba, imeshuka kutokana na kupungua...

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

error: Content is protected !!