MBUNGE wa Bunda Mjini, Ester Bulaya amemtaka Rais John Magufuli kumfukuza kazi Waziri wa Sera, Bunge, Ajira, Vijana, na Walemavu, Jenista Mhagama, kwa sababu ya kutunga kanuni mpya ya kikokotoo cha mafao ya wastaafu ambayo ilikuwa mwiba kwa wafanyakazi. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).
Mwishoni mwa mwaka jana Rais Magufuli alifuta kanuni hiyo ambayo ilikuwa inaelekeza wastaafu kulipwa asilimia 25 ya mafao yao wanapostaafu na asilimia 75 inayobakia kila mwezi, na kuagiza kikokotoo cha zamani cha malipo ya asilimia 50 ya mafao wanapostaafu, na asilimia 50 inayobakia kila mwezi kitumike katika kipindi cha mpito hadi mwaka 2023.
Akizungumza na wanahabari leo tarehe 2 Januari 2019, Bulaya ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana na Walemavu, amesema Waziri Jenista ndiye alipigia debe kanuni hiyo bungeni, na kumtaka kujiuzulu mwenyewe .
“Morali kazini zimeshuka sababu ya mtu mmoja halafu bado yupo ofisini is not fair ‘sio haki’. Dada yangu namheshimu ila anapaswa kuwajibika katika hili sina chuki nae,” amesema Bulaya.
Leave a comment