Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mwinyi: Nitakuja na staili ya Rais Magufuli
Habari za Siasa

Dk. Mwinyi: Nitakuja na staili ya Rais Magufuli

Spread the love

DAKTARI Hussein Ali Mwinyi, Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika Uchaguzi Mkuu wa Rais wa Zanzibar,  Oktoba 2020, ameahidi kufuata nyayo za Rais John Pombe Magufuli, katika mapambano ya rushwa, uzembe na ubadhirifu. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Dk. Mwinyi ametoa ahadi hiyo mbele ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM unaofanyika leo Jumamosi tarehe 11 Julai 2020, jijini Dodoma wakati akiwasalimia wajumbe hao.

Waziri huyo wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa amesema, endapo atachaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar, upole wake atauweka pembeni na kufuata ukali wa Rais Magufuli, katika kushughulikia wala rushwa, wabadhirifu na watumishi wazembe.

“Wako waliosema mimi ni mpole, lakini nimejifunza kutoka kwako mambo ya msingi, rushwa, uzembe na ubadhirifu yanataka uwe mkali na hilo nawaahidi endapo nitachaguliwa kuwa rais, nitakuja na staili ya Rais Magufuli katika maeneo hayo,” ameahidi Dk. Mwinyi .

Dk. Mwinyi amesema, endapo atafanikiwa kuwa Rais wa Zanzibar, atakuwa kiongozi bora kutokana na uzoefu alioupata akiwa waziri chini ya Rais Magufuli na marais wastaafu.

“Katika kipindi hiki cha miaka mitano ya Rais Magufuli, ameendelea kuwa nami kama waziri wake wa ulinzi, jambo limenifanya niwe nakamilisha miaka 11 kama waziri wa ulinzi.”

“Niseme pia nimejifunza mengi kutoka kwako, umenifanya nijifunze mengi katika uongozi na nidiriki kusema huko ninakokwenda nitakuwa kiongozi bora kwa sababu ya kujifunza kwako,” amesema Dk. Mwinyi.

Aidha, Dk. Mwinyi amewashukuru marais wastaafu, Jakaya Kikwete, Benjamini Mkapa na Baba yake, Ali Hassani Mwinyi kwa kumuamini na kumpa nafasi ya juu ya uongozi katika serikali zao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!