Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Daktari feki mbaroni Dodoma
Habari Mchanganyiko

Daktari feki mbaroni Dodoma

Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto
Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Dodoma linamshikilia mkazi wa Gairo mkoani Morogoro, Hassan Abdallah kwa tuhuma za kufanya kazi ya kitabibu pasipo kuwa na taaluma ya kazi hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na wanahabari Kamanda wa Polisi Dodoma, Gilles Muroto amesema Abdallah anayetuhumiwa kuwa daktari feki katika hospitali za wilaya ya Chemba mkoani Dodoma, alipohojiwa alisema anaipenda taaluma hiyo.

Kamanda Mulloto amesema mtuhumiwa huyo alikuwa anatoa huduma mbalimbali za upasuaji kwa wagonjwa wenye uvimbe, ambapo alianza kufanya upasuaji huo katika zahanati binafsi

“Tumemkamata akijihusisha na utoaji huduma mbalimbali za kitabibu na upasuaji mdogo kwa wananchi wenye uvimbe, tunaendelea kuchunguza kwa nini anafanya hivyo, tulipomhoji amesema alikuwa anafanya kwenye zahanati binafsi amekuwa akipenda taaluma hiyo ambapo anafanya hivyo pasipo kibali,” amesema Kamanda Muroto.

Kamanda Muroto amesema wanaendelea kumuhoji Abdallah na kwamba upelelezi ukikamilika atafikishwa mahakamani.

“Tunamhoji tutamfikisha mahakamani. Hatuna nafasi ya utapeli kwenye mkoa wangu udaktari feki hauna nafasi, wananchi watoe taarifa za kutosha,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!