Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Daktari feki mbaroni Dodoma
Habari Mchanganyiko

Daktari feki mbaroni Dodoma

Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto
Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Dodoma linamshikilia mkazi wa Gairo mkoani Morogoro, Hassan Abdallah kwa tuhuma za kufanya kazi ya kitabibu pasipo kuwa na taaluma ya kazi hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na wanahabari Kamanda wa Polisi Dodoma, Gilles Muroto amesema Abdallah anayetuhumiwa kuwa daktari feki katika hospitali za wilaya ya Chemba mkoani Dodoma, alipohojiwa alisema anaipenda taaluma hiyo.

Kamanda Mulloto amesema mtuhumiwa huyo alikuwa anatoa huduma mbalimbali za upasuaji kwa wagonjwa wenye uvimbe, ambapo alianza kufanya upasuaji huo katika zahanati binafsi

“Tumemkamata akijihusisha na utoaji huduma mbalimbali za kitabibu na upasuaji mdogo kwa wananchi wenye uvimbe, tunaendelea kuchunguza kwa nini anafanya hivyo, tulipomhoji amesema alikuwa anafanya kwenye zahanati binafsi amekuwa akipenda taaluma hiyo ambapo anafanya hivyo pasipo kibali,” amesema Kamanda Muroto.

Kamanda Muroto amesema wanaendelea kumuhoji Abdallah na kwamba upelelezi ukikamilika atafikishwa mahakamani.

“Tunamhoji tutamfikisha mahakamani. Hatuna nafasi ya utapeli kwenye mkoa wangu udaktari feki hauna nafasi, wananchi watoe taarifa za kutosha,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

Habari Mchanganyiko

TPF-NET Arusha yaonya jamii ya wafugaji zinazoendeleza ukatili wa watoto na wanawake

Spread the love  MTANDAO wa Polisi wanawake wa Arusha kuelekea siku 12...

Habari Mchanganyiko

Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Greyhorse zasaini mkataba wa bil.7.4

Spread the loveTAASISI ya Mwalimu Nyerere (MNF) imesaini mkataba wa miaka 10...

error: Content is protected !!