Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Channel Ten yawekwa kiporo
Habari Mchanganyiko

Channel Ten yawekwa kiporo

Neville Meena, Katibu wa Jukwaa la Wahariri Tanzania
Spread the love

JUKWAA la Wahariri Tanzania (TEF) limekiweka kiporo kituo cha Televisheni cha Channel Ten kwa kukiuka makubaliano ya kutoandika wala kutangaza habari zinazomuhusu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, anaandika Hamisi Mguta.

Katibu wa Jukwaa hilo, Neville Meena leo ameeleza kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari amesema TEF inakiri kutangazwa kwa habari za Mkuu wa mkoa huyo zaidi ya mara moja na imekuwa kawaida kwa vyombo vya Sahara Media (Star TV na Radio Free Afrika) kwa kuzingatia kwamba kufanya hivyo ni kukiuka makubaliano na mshikamano wa kitaaluma.

“Uongozi wa Jukwaa unalifanyia kazi hili ikiwa ni pamoja na kuwasiliana na taasisi husika na baadaye utatoa taarifa rasmi kuhusu matokeo ya mchakato huo, kwasasa tunawakumbusha wahariri na waandishi kwamba makubaliano yetu ya kutotangazwa kwa habari zozote zinazomuhusu Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam bado yapo palepale,” amesema Meena.

Aidha amesema aliyefungiwa kutotangazwa habari zake ni Mkuu wa mkoa na si habari za mkoa  wa Dar es Salaam hivyo habari zinazohusu matatizo, changamoto na maendeleo na maendeleo ya wananchi zinaweza kuandikwa.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!