Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yazindua Sera mbadala ya maendeleo ya Taifa
Habari za Siasa

Chadema yazindua Sera mbadala ya maendeleo ya Taifa

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimezindua sera mbadala ya Taifa leo Jumanne tarehe 25 Septemba, 2018.

Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Freeman Mbowe amesema hii ni mara ya pili kwa chama chake kuandaa na kuzindua sera mbadala ya taifa tangu kuanzishwa kwa chama hicho mwaka 1992.

“Mwanzoni mwa mwaka 1990 waasisi wa chama hiki, mimi nikiwa ni mmoja wao na ndio nilikuwa mdogo kuliko wote, tuliona siasa za ujamaa ambazo ndiyo ilikuwa sera ya CCM, hazifai na haziwezi kuwapelekea maendeleo Watanzania. Kwa pamoja tukaamua njia pekee ni kuanzisha vuguvugu la vyama vingi tukiamini kama serikali itakubali, basi tuanzishe chama cha siasa ambacho kitakuwa na sera mbadala ya ile ya ujamaa.

“Kwa hiyo mfumo wa vyama vingi ulikubaliwa, haraka tulisajili chama cha siasa cha CHADEMA na ilipofika mwaka 1993, mara tu ya kupata cheti cha usajili, tuliandaa Sera mbadala ya taifa ya mlengo wa kati ambayo ilikuwa inatofautia na ile ya ujamaa,” alisema Mbowe.

Mwenyekiti huyo ambaye ni Mbunge wa jimbo la Hai, amesema baada ya kuiandaa sera ya chama chao, walimpelekea Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ambaye baada ya kuisoma aliikubali na kusema kuwa sera hiyo ndiyo hasa italeta maendeleo kwa Watanzania.

Akizungumza mbele ya wajumbe wa kamati kuu ya Chadema wakiwemo Mawaziri wakuu wastaafu, Frederick Sumaye na Edward Lowassa, Wabunge wanaotokana na chama hicho, wageni waalikwa wakiwemo mabalozi wa nchi mbalimbali na wananchi wa kawaida, Mbowe alisema baada ya miaka 25, chama chake kimeamua kuandaa tena sera mbadala ya taifa.

“Chama changu kimeamua kuandaa tena Sera hizi ambazo tumegusia Nyanja 12 ambazo tuna Imani zina tija kwa maslahi mapana ya wananchi na taifa kwa ujumla wake.

“Tumegusia Katiba, Utawala, Uchumi wa Soko Jamii, Siasa za ndani, Siasa za Kijamii na Afya. Lakini pia tumeangazia kwenye masuala ya Usimamizi wa ardhi, Kilimo, Miundombinu, Mazingira na mambo ya nje. Na hii sera yetu tunaiweka wazi kwa umma ili Watanzania wajue nini tunachokipigania kwenye hii nchi,” aliongeza Mbowe.

Baada ya kuzindua Sera hiyo, Mbowe amesema chama chake kimefungua rasmi milango ya kupokea maoni na ushauri juu ya sera hiyo kutoka kwenye vyama vya siasa, mashirika ya umma, taasisi mbalimbali na raia wa kawaida.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!