Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema: Tuwasindikize mawakala vituoni 
Habari za Siasa

Chadema: Tuwasindikize mawakala vituoni 

Tundu Lissu, Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chadema
Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) nchini Tanzania,  kimewaomba wanachama wake kuwasindikiza mawakala wa chama hicho katika vituo vya kupigia kura. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Uchaguzi Mkuu wa madiwani, wabunge na Rais nchini Tanzania utafanyika kesho Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020.

Wito huo umetolewa leo Jumanne tarehe 27 Oktoba 2020 na Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika wakati akizungumza katika ufungaji kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania wa chama hicho, Tundu Lissu katika Uwanja wa Tanganyika Packres jijini Dar es Salaam.

“Mimi nina uzoefu wa ninyi wananchi wa Dar es Salaam, mnakawaida ya kuchelewa kupiga kura, tume imetangaza kufungua vituo saa 1:00 asubuhi, tafadhali fika saa 12:00 asubuhi kamili ,sababu wakala wetu wanawapangia njama za kutowaingiza. Akifika saa 12 asubuhi asiwe peke yake asindikizwe na wananchi kuhakikisha anaingia ndani,” amesema Mnyika.

John Mnyika, Katibu Mkuu wa Chadema

Mnyika amewaomba wafuasi wa chama hicho kubaki katika vituo vya kupigia kura kusubiri matokeo yake.

“Imetolewa kauli na IGP Simon Sirro jana na leo akiwasisitiza kwamba tukipiga kura twende nyumbani, kauli iliyotolewa na mgombea wa CCM, nasema wazi na Polisi wasikie tukipiga kura hakuna kurudi nyumbani tushuhudie kazi akiendelea,” amesema Mnyika.

Mnyika amewataka wasimamizi wa uchaguzi kila mahali, watoe nakala za matokeo ngazi ya kata majimbo ili mawakala wabaki na uthibitisho wa matokeo ya uchaguzi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!