CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) nchini Tanzania, kimewaomba wanachama wake kuwasindikiza mawakala wa chama hicho katika vituo vya kupigia kura. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Uchaguzi Mkuu wa madiwani, wabunge na Rais nchini Tanzania utafanyika kesho Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020.
Wito huo umetolewa leo Jumanne tarehe 27 Oktoba 2020 na Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika wakati akizungumza katika ufungaji kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania wa chama hicho, Tundu Lissu katika Uwanja wa Tanganyika Packres jijini Dar es Salaam.
“Mimi nina uzoefu wa ninyi wananchi wa Dar es Salaam, mnakawaida ya kuchelewa kupiga kura, tume imetangaza kufungua vituo saa 1:00 asubuhi, tafadhali fika saa 12:00 asubuhi kamili ,sababu wakala wetu wanawapangia njama za kutowaingiza. Akifika saa 12 asubuhi asiwe peke yake asindikizwe na wananchi kuhakikisha anaingia ndani,” amesema Mnyika.
Mnyika amewaomba wafuasi wa chama hicho kubaki katika vituo vya kupigia kura kusubiri matokeo yake.
“Imetolewa kauli na IGP Simon Sirro jana na leo akiwasisitiza kwamba tukipiga kura twende nyumbani, kauli iliyotolewa na mgombea wa CCM, nasema wazi na Polisi wasikie tukipiga kura hakuna kurudi nyumbani tushuhudie kazi akiendelea,” amesema Mnyika.
Mnyika amewataka wasimamizi wa uchaguzi kila mahali, watoe nakala za matokeo ngazi ya kata majimbo ili mawakala wabaki na uthibitisho wa matokeo ya uchaguzi huo.
Leave a comment