Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema: Mdude amejeruhiwa kichwani
Habari za Siasa

Chadema: Mdude amejeruhiwa kichwani

John Mrema, Mkurugenzi wa Itifaki na Mawasiliano wa Chadema
Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeeleza maendeleo ya afya ya mwanachama wake Mdude Nyagali, amejeruhiwa kichwani. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Kwa sasa, Mdude amelazwa kwenye Hospitali ya Rufaa Mbeya akipatiwa matibabu ya majeraha aliyopata, baada ya kutekwa na kuteswa na watu wasijojulikana.

Akizungumza na Wanahabari leo tarehe 9 Mei 2019 jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje, John Mrema amesema, majira ya asubuhi Mdude aliingizwa katika chumba cha upasuaji kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji.

Mrema amesema, Mdude aliyepatikana jana tarehe 8 Mei 2019 baada ya kuachwa na watu wasiojulikana, amefanyiwa vipimo mbalimbali ikiwemo cha CT Scan na kubainika kwamba, amepata matatizo maeneo ya kichwani.

“Madaktari wananedelea na vipimo na uchunguzi wa afya yake katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya asubuhi ameingizwa chumba cha upasuaji baada ya vipimo vya CT Scan kwenye kichwa.

“Madaktari wamempeleka moja kwa moja kwenye chumba cha upasuaji, labda watatoa taraifa za kitaalamu hapo baadaye,” amesema Mrema.

Amesema, kabla ya Mdude kupelekwa katika chumba cha upasuaji, alihojiwa na maafisa wa polisi kuhusu tukio la kutekwa kwake na watu wasiojulikana.

“Tangu leo asubuhi saa 12.00 polisi wa vyeo mbalimbali walikwenda hospitalini na kutaka kumhoji pamoja na kwamba ufahamu wake haukurudi vizuri na walitaka taarifa ili waweze kukamata watekaji, wa kwanza ni RPC  na RCO wa Mbeya,” amesema Mrema na kuongeza.

“Baada ya dakika chache alifika OCD  wa Mbeya Mjini na wao walichofanya walifanya mahojiano lakini baada ya muda saa tatu asubuhi RCO wa mkoa wa Songwe akiongozana na timu ya wapelelezi, walifika hospitalini wakamhoji na kuchukua maelezo yake pamoja kwamba, anaongea kwa tabu walichukua wanayokumbuka,”amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!