Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM yateua mgombea Jimbo la Nasari
Habari za Siasa

CCM yateua mgombea Jimbo la Nasari

John Pallangyo ameteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) mgombea wa Ubunge jimbo la Arumelu Mashariki
Spread the love

JOHN Pallangyo ameteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kugombea ubunge katika Jimbo la Arumeru Mashariki lililokuwa likisimamiwa na Joshua Nasari wa Chadema. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole, Pallangyo ameteuliwa leo tarehe 15 Aprili 2019 na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) iliyoketi jijini Dodoma.

Pallangyo kupitia tiketi ya CCM anatarajiwa kugombea ubunge katika jimbo hilo baada ya Nasari kutenguliwa ubunge wake na Ofisi ya Bunge.

Halmashauri hiyo iliyoongozwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais John Magufuli, pia imefanya uteuzi wa wajumbe wanaogombea ujumbe wa NEC kupiti Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM) kundi la bara.

Wajumbe walioteuliwa kugombea ujumbe wa NEC ni pamoja na Sara Joel Sompo, Japhary Kabecha Mghamba na Ngusa Charles Juda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!