Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa CCM yateua mgombea Jimbo la Nasari
Habari za Siasa

CCM yateua mgombea Jimbo la Nasari

John Pallangyo ameteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) mgombea wa Ubunge jimbo la Arumelu Mashariki
Spread the love

JOHN Pallangyo ameteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kugombea ubunge katika Jimbo la Arumeru Mashariki lililokuwa likisimamiwa na Joshua Nasari wa Chadema. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole, Pallangyo ameteuliwa leo tarehe 15 Aprili 2019 na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) iliyoketi jijini Dodoma.

Pallangyo kupitia tiketi ya CCM anatarajiwa kugombea ubunge katika jimbo hilo baada ya Nasari kutenguliwa ubunge wake na Ofisi ya Bunge.

Halmashauri hiyo iliyoongozwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais John Magufuli, pia imefanya uteuzi wa wajumbe wanaogombea ujumbe wa NEC kupiti Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM) kundi la bara.

Wajumbe walioteuliwa kugombea ujumbe wa NEC ni pamoja na Sara Joel Sompo, Japhary Kabecha Mghamba na Ngusa Charles Juda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!