Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM yateua mgombea Jimbo la Nasari
Habari za Siasa

CCM yateua mgombea Jimbo la Nasari

John Pallangyo ameteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) mgombea wa Ubunge jimbo la Arumelu Mashariki
Spread the love

JOHN Pallangyo ameteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kugombea ubunge katika Jimbo la Arumeru Mashariki lililokuwa likisimamiwa na Joshua Nasari wa Chadema. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole, Pallangyo ameteuliwa leo tarehe 15 Aprili 2019 na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) iliyoketi jijini Dodoma.

Pallangyo kupitia tiketi ya CCM anatarajiwa kugombea ubunge katika jimbo hilo baada ya Nasari kutenguliwa ubunge wake na Ofisi ya Bunge.

Halmashauri hiyo iliyoongozwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais John Magufuli, pia imefanya uteuzi wa wajumbe wanaogombea ujumbe wa NEC kupiti Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM) kundi la bara.

Wajumbe walioteuliwa kugombea ujumbe wa NEC ni pamoja na Sara Joel Sompo, Japhary Kabecha Mghamba na Ngusa Charles Juda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!