Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Butiku atamani uchaguzi mkuu uwe huru, amani
Habari za Siasa

Butiku atamani uchaguzi mkuu uwe huru, amani

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku
Spread the love

TAASISI ya Mwalimu Nyerere imesema, Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 ukiwa wa amani, huru na haki utawezesha kupatikana viongozi bora. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Taasisi hiyo, Joseph Butiku wakati akitoa salamu za taasisi kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) unaofanyika ukumbi wa Mlimani City Dar es Salaam.

“Nawashukuru kwa mwaliko wa kunikaribisha mimi kwa niaba ya Taasisi ya Mwalimu Nyerere.”

“Nimekuja kuwaona mlivyo, mmependeza. Mwenyekiti (Freeman Mbowe) unapendeza,” amesema Butiku huku akishangiliwa na wajumbe wa mkutano mkuu

Amesema, Taifa letu linadumu katika amani, Taifa letu linapata maendeleo ya watu kutokana na juhudi zao wenyewe kwa njia za kujitegemea.

“Taifa letu lina miaka 59. Utaratibu huu wa vyama vingi ni miaka 28. Tulipata uhuru ili tujitawale, ili tujisimamie mambo yetu wenyewe na utaratibu wa vyama vingi ulianzishwa ili kuboresha utawala bora na kuendesha nchi kujumuisha wananchi wote.”

“Tumedumu katika utamaduni huo kwa changamoto zilizokuwepo. Sisi kwenye taasisi siyo wanasiasa ila tunapenda kushauri, ili tupate viongozi wote tuzingatie sheria inayolinda mambo haya na taratibu zote,” amesema Butiku.

Mwenyekiti huyo amesema “bahati mbaya, tunayumba kidogo lakini uchaguzi wa mwaka huu utaonyesha uhuru, wazi na wa haki.”

“Uchaguzi ukiwa hivyo, utatupatia viongozi bora na viongozi hao walinde msingi wa Taifa letu wanadumu katika usawa na Taifa linadumu katika haki kwa wote,” amesema

Akihitimisha salamu zake, Butiku amesema “nawatakieni mkutano mwema. Rafiki yangu (Tundu) Lissu tulikutana zamani tulipokuwa tunazungumza mambo ya nchi” naona uko imara. Kauli hiyo ilimfanya Lissu aliyekuwa kando yake kutabasamu huku wajumbe wakishangilia

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!