Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msajili avitaka vyama vya siasa kuzingatia sheria
Habari za Siasa

Msajili avitaka vyama vya siasa kuzingatia sheria

Msajili msaidizi wa vyama vya siasa, Sisty Nyahonza
Spread the love

OFISI ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tazania, umetoa wito kwa vyama vya siasa nchini humo kuhakikisha wanazingatia sheria na taratibu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Msajili msaidizi wa vyama vya siasa, Sisty Nyahonza mbele ya wajumbe wa mkutano mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) unaofanyika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.

Hata hivyo, Nyahoza amekutana na kauli za wajumbe zilizokuwa zikikatisha hotuba yake.

“Nimehudhuria mkutano huu mara kadhaa na nipo hapa kumwakilisha msajili wa vyama na sisi tunakuja hapa kutekeleza wajibu wetu wa kisheria wa vyama vyote,” amesema Nyahoza huku sauti zikisikika zikisema ‘mbona msajili mwenyewe hatumwoni’

Akiendelea, Nyahoza amesema “ili kuhakikisha mikutano yenu inafanyika kwa kuzingatia sheria na kanuni. Kwenye haki kuna wajibu ikiwemo kusimamia sheria za nchi.”

Kisha sauti zikasikika zikisema ‘mbona kuna sheria mbovu.’

“Mwenyekiti (Freeman Mbowe), moja wapo ya misingi muhimu ya chama cha siasa, kama mnavyosema mnatetea demokrasia, msingi muhimu ni demokrasia ndani ya chama na demokrasia ni sehemu ya watu kuheshimu sheria.”

Akihitimisha hotuba yake, Nyahoza amesema “wito wetu kama ofisi ya msajili na mlezi, ninyi na vyama vyote mheshimu sheria na tunashauri tuheshimu sheria, tufanye uchaguzi kwa uhuru, haki na amani.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!