Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge lazidi kuikaanga serikali ya Magufuli
Habari za SiasaTangulizi

Bunge lazidi kuikaanga serikali ya Magufuli

Rais John Magufuli (kulia) akiteta jambo na Spika wa Bunge, Job Ndugai
Spread the love

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, imetoa mapendekezo 19 kwa serikali, yanayohitaji kufanyiwa kazi haraka iwezekanavyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Miongoni mwa mapendekezo yaliyotolewa na serikali, ni kilio cha ucheleweshaji katika utoaji wa fedha za miradi ya maendeleo kama zilivyoidhinishwa na Bunge. Baadhi ya maeneo yaliyotajwa, ni sekta za kilimo, uvuvi na maji.

Akizungumza wakati wa akiwasisha taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, mwenyekiti wa kamati hiyo, Mahamoud Mgimwa alisema, kitendo cha serikali cha kuchelewesha au kutopekeka kabisa fedha za maendeleo, kumesababisha matatizo makubwa kwa wananchi.

“Serikali haiwezi kuaminika mbele ya macho ya jamii, ikiwa haitatekeleza kwa vitendo ahadi yake ya kupelekaji fedha za maendeleo katika sekta muhimu kwa uhai wa wananchi wake,” ameeleza Mgimwa.

Alisema, “wala serikali haiwezi kuaminika ikiwa inatoza kodi hata kwenye bidhaa za maziwa na ikiwa haikumarisha ununuzi wa zao la korosho.”

Pamoja na mapendekezo hayo, Kamati ya Mgimwa imetaka serikali kuhakikisha kuwa fedha za bajeti ambazo zimepitishwa na Bunge zinapelekwa kunakohusika kama ilivyoahi bungeni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!