Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge kuanza, taarifa ya CAG kuchambuliwa
Habari za Siasa

Bunge kuanza, taarifa ya CAG kuchambuliwa

Bunge la Tanzania
Spread the love

VIKAO vya Kamati 14 za Kudumu za Bunge, vinatarajia kuanza tarehe 21 Oktoba 2019 hadi Novemba Mosi mwaka huu. Anaripoti Hamisi Mguta…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 16 Oktoba 2019 na Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa cha Ofisi ya Bunge.

Taarifa hiyo imeleeza kuwa, miongoni mwa shughuli zitakazofanyika katika vikao hivyo, ni uchambuzi wa Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kuhusu hesabu zilizokaguliwa za Serikali za Mitaa na Serikali Kuu.

Pia, Kamati hizo zitafanya uchambuzi wa Taarifa ya Msajili wa Hazina kuhusu uwekezaji wa mitaji ya umma katika mashirika na taasisi mbalimbali nchini.

Na uchambuzi wa Sheria ndogo zilizowasilishwa wakati wa mkutano mkuu wa kumi na sita wa Bunge.Pamoja na Kupokea na kujadili taarifa ya mapendekezo ya mwongozo wa kutayarisha Mpango wa Maendeleo wa Taifa na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2020/2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!