Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bobi Wine aswekwa rumande
Habari Mchanganyiko

Bobi Wine aswekwa rumande

Bobi Wine
Spread the love

MBUNGE wa Kyadondo Mashariki nchini Uganda, Robert Kyagulanyi ‘Bobi Wine’ amewekwa rumande katika Kituo cha Polisi cha Naggalama, akituhumiwa kuandaa maandamano ya umma kinyume cha sheria. Inaripoti Mitandao ya Kijamii…(endelea).

Kwa mujibu wa mitandao ya kimataifa, Bobi Wine anashikiliwa na Jeshi la Polisi nchini Uganda tangu tarehe 29 Aprili 2019, na kwamba hatima ya dhamana yake itajulikana tarehe 2 Mei 2019.

Ofisa wa Polisi nchini Uganda, Fred Ennanga amesema Bobi Wine anazuiwa na polisi na kwamba uchunguzi wa tuhuma zake unaendelea. Amesema Mwanasiasa huyo aliongoza maandamano hayo pasipo kuomba ruhusa kutoka kwa polisi.

Bobi Wine anasota rumande ikiwa ni siku chache baada ya kuwekwa kizuizini na Jeshi la Polisi nyumbani wake. Mwanasiasa huyo anatarajiwa kupelekwa katika gereza la Luzira mjini Kampala.

Mwanasiasa huyo mpinzani nchini Uganda anatuhumiwa kuongoza maandamano hayo ya kupinga kodi ya kutumia mitandao ya kijamii, mwaka jana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!