Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bobi Wine aswekwa rumande
Habari Mchanganyiko

Bobi Wine aswekwa rumande

Bobi Wine
Spread the love

MBUNGE wa Kyadondo Mashariki nchini Uganda, Robert Kyagulanyi ‘Bobi Wine’ amewekwa rumande katika Kituo cha Polisi cha Naggalama, akituhumiwa kuandaa maandamano ya umma kinyume cha sheria. Inaripoti Mitandao ya Kijamii…(endelea).

Kwa mujibu wa mitandao ya kimataifa, Bobi Wine anashikiliwa na Jeshi la Polisi nchini Uganda tangu tarehe 29 Aprili 2019, na kwamba hatima ya dhamana yake itajulikana tarehe 2 Mei 2019.

Ofisa wa Polisi nchini Uganda, Fred Ennanga amesema Bobi Wine anazuiwa na polisi na kwamba uchunguzi wa tuhuma zake unaendelea. Amesema Mwanasiasa huyo aliongoza maandamano hayo pasipo kuomba ruhusa kutoka kwa polisi.

Bobi Wine anasota rumande ikiwa ni siku chache baada ya kuwekwa kizuizini na Jeshi la Polisi nyumbani wake. Mwanasiasa huyo anatarajiwa kupelekwa katika gereza la Luzira mjini Kampala.

Mwanasiasa huyo mpinzani nchini Uganda anatuhumiwa kuongoza maandamano hayo ya kupinga kodi ya kutumia mitandao ya kijamii, mwaka jana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!