Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Airbus A220-300 iliyokamatwa Afrika Kusini yatua Tanzania
Habari za SiasaTangulizi

Airbus A220-300 iliyokamatwa Afrika Kusini yatua Tanzania

Spread the love

NDEGE ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), iliyokuwa imeshikiliwa nchini Afrika Kusini, tayari imetua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Ndege hiyo iliyokuwa imeshikiliwa kwa amri ya Mahakama Kuu ya Gauteng, Johannesburg imewasili JNIA tarehe 4 Septemba 2019 saa 2:25 usiku.

Kushikiliwa kwa ndege hiyo kulitokana na kesi ya fidia iliyofunguliwa mahakamani hapo na Hermanus Steyn dhidi ya Serikali ya Tanzania.

Katika kesi hiyo, raia huyo wa Afrika Kusini alieleza kuwa anaidai serikali ya Tanzania malipo yaliyobaki ya fidia ya mali zake zilizotaifishwa mwaka 1982.

Akipokea ndege hiyo JNIA, Profesa Palamagamba Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje alieleza furaha yake ambapo alisema, “Ni faraja kwa nchi kushinda kesi.”

Prof. Kabudi amewapongeza majaji wa Afrika Kusini kusimamia haki uliowezesha ndehe hiyo kuachwa huru na kurejea nchini. Hata hivyo ameeleza kutokuwa na wasiwasi wowote kwa ndege za Tanzania kukamatwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!