Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo yaibomoa CUF Tanga kimya kimya
Habari za SiasaTangulizi

ACT-Wazalendo yaibomoa CUF Tanga kimya kimya

Spread the love

CHAMA cha Wananchi (CUF), kipo kwenye wakati mgumu baada ya ACT-Waalendo kuendelea kubomoa ngome zake. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Licha ya kauli tata kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kwamba, kinaweza kufutwa, chama hicho kimeendelea kupokea waliokuwa wanachama wa CUF kwenye maeneo mbalimbali ya nchi.

Katika jiji la Tanga, Kata ya Duga mamia ya waliokuwa wanachama wa CUF wamechukua kadi za ACT-Wazalendo kwa madai ya kuchoshwa na mwenendo wa Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CUF-Taifa na viongozi wengine wa chama hicho.

“Simuelewi Prof. Lipumba na viongozi wenzake, lakini nimechoshwa na mwenendo wa CUF. Naamini katika demokrasia ndio maana najiunga na ACT-Wazalendo,” amesema Godfrey Simon baada ya kuchukua kati ya CUF.

Kutokana na kazi inayofanywa na waliokuwa viongozi wa CUF baada ya kujiunga na ACT-Wazalendo, Ismail Jussa, aliyekuwa kiongozi mwandamizi wa CUF ameandika kwenye ukursa wake wa twetter akiwapongeza viongozi hao kwa kazi ya usajili wa wanachama wapya kutoka CUF.

“Mpambanaji Rashid Jumbe Hamza akiwaongoza waliokuwa wanachama wa CUF wa Kata ya Duga, Mkoa wa Tanga kushusha tanga na kupandisha tanga ili safari iendelee. ACT-Wazalendo ndiyo habari ya mjini,” ameandika Jussa.

Ado Shaibu, Katibu Mwenezi na Mawasiliano ya Umma wa chama hicho ameuambia mtandao wa MwanaHALISI ONLINE kuwa, shughuli za chama hicho hazijakwamishwa na chochote na kwamba, uimara wa hali ya juu wa ACT-Wazalendo sasa unadhihiri.

“Tanga na maeneo mengine ya nchi kazi inaendelea kama ilivyopangwa, wanachama wanaendelea kujiunga. Wao wenyewe wamefurahia ACT-Wazalendo, wamefurahia Maalim Seif Sharif Hamad kuhamia chama hiki,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!