Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri wa Madini afunga mgodi Pwani
Habari za Siasa

Waziri wa Madini afunga mgodi Pwani

Spread the love

SERIKALI imesimamisha shughuli za mgodi unaochimbwa madini ya Kaolin unaomilikiwa na kampuni ya RAK Kaolin kutokana na kutoridhishwa na mwenendo wa uendeshaji wake na biashara ya madini hayo viwandani. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Agizo hilo lilitolewa jana na Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uchimbaji madini ya ujenzi Julai 25,2018.

Waziri Nyongo alitoa agizo hilo baada ya kutoridhishwa na shughuli za mgodi huo uliopo katika Kijiji cha Kimani wilayani Kisarawe mkoani Pwani, ikiwemo umiliki wa ardhi, leseni ya mgodi, uchimbaji pamoja na biashara ya madini hayo viwandani.

Waziri Nyongo alisema shughuli za uchimbaji na biashara ya madini katika mgodi huo hazioneshi wazi taratibu za ulipaji serikalini, mrabaha na tozo mbalimbali zilizowekwa kwa mujibu wa sheria.

Aidha, alimtaka mmiliki wa leseni ya mgodi huo kuwasilisha wizara ya madini nakala ya mkataba walioingia kati yake na wachimbaji wa madini ya Kaolin katika mgodi huo, na namna ambavyo aliweza kumiliki eneo husika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!