SERIKALI imesimamisha shughuli za mgodi unaochimbwa madini ya Kaolin unaomilikiwa na kampuni ya RAK Kaolin kutokana na kutoridhishwa na mwenendo wa uendeshaji wake na biashara ya madini hayo viwandani. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Agizo hilo lilitolewa jana na Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uchimbaji madini ya ujenzi Julai 25,2018.
Waziri Nyongo alitoa agizo hilo baada ya kutoridhishwa na shughuli za mgodi huo uliopo katika Kijiji cha Kimani wilayani Kisarawe mkoani Pwani, ikiwemo umiliki wa ardhi, leseni ya mgodi, uchimbaji pamoja na biashara ya madini hayo viwandani.
Waziri Nyongo alisema shughuli za uchimbaji na biashara ya madini katika mgodi huo hazioneshi wazi taratibu za ulipaji serikalini, mrabaha na tozo mbalimbali zilizowekwa kwa mujibu wa sheria.
Aidha, alimtaka mmiliki wa leseni ya mgodi huo kuwasilisha wizara ya madini nakala ya mkataba walioingia kati yake na wachimbaji wa madini ya Kaolin katika mgodi huo, na namna ambavyo aliweza kumiliki eneo husika.
Leave a comment