Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto amtaka JPM urais 2020
Habari za SiasaTangulizi

Zitto amtaka JPM urais 2020

Spread the love

ZITTO Kabwe ameeleza dhamira yake ya kutaka kupambana na Dk. John Magufuli, katika kugombea urais kwenye uchaguzi wa Oktoba mwaka huu. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Amesema, anatamani vyama vya upinzani vimuunge mkono kwenye uchaguzi huo ili akabiliano na Dk. Magufuli kama atateuliwa na chama chake – Chama Cha Mapinduzi (CCM) – kugombea urais kwenye uchaguzi huo.

Zitto ambaye ni Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, ametoa kauli hiyo leo tarehe 18 Februari 2020, wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.

Amesema, katika mazingira ya sasa, ndoto yake hiyo itafanikiwa endapo vyama vya upinzani vitakubali kumuunga mkono katika harakati hiyo.

“Mimi kama Zitto nautaka urais kama chama kitakubali.  Lakini kwa mazingira ya Tanzania, lazima tuwe na mgombea anayeungwa na vyama vya upinzani, ukivuka kwenye chama chako, uanenda kwenye kigingi kingine. Kama vyama vikiona naweza kupeperusha bendera kwa niaba yao, sitakataa,” amesema Zitto.

Pia amesema, kama vyama vya siasa vya upinzani havitampa ridhaa ya kugombea nafasi hiyo, atatoa ushirikiano kwa mtu atakayeteuliwa kugombea urais katika uchaguzi huo.

“Lakini pili, wenzangu wakiona kuna mwanachama mwingine wa upinzani tunaona anafaa kubeba bendera na kugombea, mimi namuunga mkono,” amesema.

Mbunge huyo wa Kigoma Mjini amesema, ndoto yake ni kuiongoza Tanzania katika misingi ya haki, usawa na demokrasia.

“Mimi nina ndoto, ningependa siku moja kuongoza nchi yangu.  Kutenda haki, kuirudisha heshima ya Tanzania kimataifa.

“Kuona haki za binadamu zinaheshimiwa na si Tanzania ukigombana na viongozi unafunguliwa mashtaka ya utakatishaji fedha. Tuwe na uhuru wa mawazo na si hofu kama ilivyo sasa hivi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!