Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yamchongea Kotei TFF
Michezo

Yanga yamchongea Kotei TFF

Spread the love

MARA baada kiungo wa Simba, James Kotei kumpiga ngumi ya mgongo mlinzi wa kushoto wa Yanga Gadiel Michael wakati wakiwania mpira kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliowakutanisha mahasimu hao wikiendi iliyopita uongozi wa Yanga waibuka na kulaani kitendo hicho ambacho kimeonekana siyo cha kiungwana. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Klabu hiyo imekwenda mbali zaidi kiasi cha kuiandikia barua Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuhusu vitendo ambavyo si vya kiungwana vilivyotokea kwenye mchezo huo ambao ulimalizika kwa suluhu uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Akiongea mbele ya waandishi wa Habari kwenye makao makuu ya klabu hiyo, Dismas Ten alisema yapo matukio kadhaa yaliyojitokeza kwenye mchezo huo yalikuwa siyo ya kiungwana ambayo kila mwanamichezo hawezi kuvumiliana.

“Sisi kama klabu tumeshaandika barua kwenda kwenye mamlaka husika ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kwa vitendo hivyo na nina amini hatua stahiki zitachukuliwa kutokana na bodi ya ligi wako imara kusimamia taratibu zinazoongoza mpira wetu,” alisema Dismas Ten.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!