Kajubi amesema waandishi wengi wa Tanzania wamekuwa wanafanya kazi katika mazingira magumu ya ufanyaji kazi zao licha ya tasnia ya habari kuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya kila siku.
Amesema mazingira magumu ya ufanyaji kazi kwa waandishi yamakuwa yakiongeza kila siku licha ya tasnia hiyo kutumika kwa kiwango kikubwa katika harakati za maendeleo ya jamii husika.
Owino Opondo, mwezeshaji katika mkutano huo, amesema kumekuwepo na mazingira ya kupigwa na kudhalilishwa kwa waandishi wa habari bila ya wahusika wanaofanya hayo kuchukuliwa hatua hali iliyojenga hofu kwa waandishi wanapofanya kazi zao.
“Kumekuwepo kwa matukio mengi dhidi ya waandishi na vyombo vyao, ikiwemo kufungwa vyombo vya habari, kutishwa, kuteshwa kwa waandishi, lakini hadi sasa hakuna wahusika waliohusika na vitendo hivyo waliokamatwa,” amesema Opondo.
Mbali hayo Opondo amesisitiza uwepo na weledi kwa waandishi wa habari kwani fani ya habari ni fani kama zilivyo fani nyingine zinazohitaji weledi katika utendaji wake wa kazi.
Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) sambamba na wafanyakazi wa...
By Mwandishi WetuDecember 11, 2023Spread the loveJeshi la polisi mkoani Kilimanjaro limekamata shehena ya dawa za...
By Mwandishi WetuDecember 11, 2023Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imeungana na Watanzania kutoa pole...
By Mwandishi WetuDecember 11, 2023Spread the loveKAMPUNI ya Amsons Group kupitia kampuni zake za Camel Oil...
By Mwandishi WetuDecember 11, 2023
Leave a comment