Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ushirikiano ndiyo silaha pekee itakayowalinda waandishi-MCT
Habari Mchanganyiko

Ushirikiano ndiyo silaha pekee itakayowalinda waandishi-MCT

Kajubi Mkajanga, Katibu Mkuu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT)
Spread the love
KAJUBI Mukajanga, Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), amesema silaha pekee itakayowakwamua waandishi wa habari nchini katika mazingira ya magumu wanayopitia ni kuongeza ushirikiano katika utendaji wa kazi zao za kila siku na kuongeza ufanisi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).Katibu Mkuu huyo ameyasema hayo leo tarehe 4 Oktoba, 2018 visiwani Zanzibar katika mkutano maalumu wa wanachama wa MCT wenye lengo la kujadili ufinyu wa vyombo vya habari katika kufanya kazi na jamii.

Kajubi amesema waandishi wengi wa Tanzania wamekuwa wanafanya kazi katika mazingira magumu ya ufanyaji kazi zao licha ya tasnia ya habari kuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya kila siku.

Amesema mazingira magumu ya ufanyaji kazi kwa waandishi yamakuwa yakiongeza kila siku licha ya tasnia hiyo kutumika kwa kiwango kikubwa katika harakati za maendeleo ya jamii husika.

Owino Opondo, mwezeshaji katika mkutano huo, amesema kumekuwepo na mazingira ya kupigwa na kudhalilishwa kwa waandishi wa habari bila ya wahusika wanaofanya hayo kuchukuliwa hatua hali iliyojenga hofu kwa waandishi wanapofanya kazi zao.

“Kumekuwepo kwa matukio mengi dhidi ya waandishi na vyombo vyao, ikiwemo kufungwa vyombo vya habari, kutishwa, kuteshwa kwa waandishi, lakini hadi sasa hakuna wahusika waliohusika na vitendo hivyo waliokamatwa,” amesema Opondo.

Mbali hayo Opondo amesisitiza uwepo na weledi kwa waandishi wa habari kwani fani ya habari ni fani kama zilivyo fani nyingine zinazohitaji weledi katika utendaji wake wa kazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!