Mchezo wa mzunguko wa 32 wa michuano ya kombe la Shirikisho la Azam, kati ya Yanga dhidi ya Mbao Fc, sasa utapigwa kwenye dimba la Ccm Kirumba Mwanza badala ya Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)
Mchezo huo ambao umepangwa kupigwa tarehe 29 Januari 2022, siku ya Juma Mosi majira ya saa 1o jioni, badala ya muda wa awali was aa 1 usiku.
Mchezo huo namba 79, umeamishiwa kwenye Uwanja wa Ccm Kirumba kufuatia Uwanja wa Benjamin Mkapa kuwa na shughuli nyingine siku ya tarehe hiyo.
Mara baada ya wenyeji wa mchezo huo klabu ya Yanga kujulishwa juu ya matumizi ya Uwanja huo siku ya Jumamosi, ndipo walipoamua kuupeleka mchezo huo jijini Mwanza ambapo kwa msimu huu hakuna timu yoyote ya Ligi Kuu.
Leave a comment